GEITA: Wanamchi Mwili wa Marehemu nyumbani kwa Mwenyekiti



GEITA: Baadhi ya Wananchi wa Mtaa wa Nyakabale wametelekeza mwili wa marehemu nyumbani kwa Mwenyekiti wa mtaa, Elias Ndarawa

Mwenyekiti Ndarawa anatuhumiwa kutoshughulikia tukio la marehemu Zacharia Shaban kupigwa na Polisi Jamii hadi kufa

Leo Machi 12, Majaliwa Shaban, ndugu wa marehemu amesema kwamba nduguye alipigwa Machi 5,2018 akiwa eneo la Mgodi wa Dhahabu Geita(GGM) akiokota mabaki ya mawe ya dhahabu maarufu magwangala

Amesema Zacharia alipelekwa Polisi alikokaa kwa siku 6 na aliporudi uraiani hali yake ilikuwa mbaya, alipelekwa hospitali alikofariki dunia Jumamosi Machi 10,2018 na hadi sasa hakuna kiongozi aliyefika kwenye msiba huo wala kutoa kauli yoyote

Mkazi wa mtaa huo, Johnson John amesema hawapo tayari kuzika hadi Serikali itakapotoa kauli kuhusu hatima ya maisha yao kwa kuwa Polisi Jamii wamekuwa wakiwapiga na kuwajeruh

Post a Comment

0 Comments